• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Baraza Maalum la kujadili hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali lafanyika Chalinze

Imewekwa: June 16th, 2022

ChalinzeDc Yafanya Baraza maalumu la kujadili Hoja za CAG.

Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kupitia kwa Baraza lake la madiwani hii leo limefaanya Baraza maalumu la kujadili hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG ikiwa ni kabla ya kukamilika kwa mwaka wa fedha wa 2021/2022.

Baraza hilo maalumu la kujadili hoja za Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ilianza kwa kusomwa kwa  ripoti ya Ukaguzi kutoka wa fedha za serikali na Mkuu wa idara ya Fedha na Biashara Ndg. Ponsian Kirumbi kwaniaba ya Mkurugenzi Mtendaji.

Mara baada ya ripoti hiyo Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Bi.Mary Kiboko ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kwakuwa na hati safi inayoridhisha kwa takribani miaka mitatu mfululizo

“Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaipongongeza Halmashauri ya Chalinze kupitia Baraza la madiwani,Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Watendaji wote kwa usimamizi mzuri wa fedha na kuhakikisha Halmashauri inapata Hati safi.

Katika Baraza hilo maalum lililohudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kwa kupata hati safi kutoka katika ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali CAG ambapo amepongeza ushirikiano wanauonyesha baina ya waheshimiwa madiwani na watendaji katika kusimamia vyema fedha za serikali na kufanya kazi kwa umoja.

Vile vile Mhe. Kunenge ameiagiza Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze pamoja Halmashauri zote kutengeneza mazingira ya kutoa elimu ya Uchumi kwa Madiwani ili waweze kuibua vyanzo vipya vya Mapato ,kuviendesha pamoja na kutafuta masoko kutoka sehemu mbalimbali.

“Naiagiza Halmashauri ya Chalinze kuwepo kwa mafunzo kwa madiwani wote juu ya masuala ya uchumi yanayohusu ubunifu,kuona fursa na kutafuta masoko na ninataka Mabaraza yote ya  madiwani katika Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kuzungumzia masuala ya uchumi kwani itasaidia kuongeza mawazo ya kuongeza kipato kwa Halmashauri na mikakaki ya kuongeza uchumi wa Chalinze na Mkoa kwa ujumla”Amesema Mhe.Kunenge.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Abdallah ameipongeza Serikali kwa hatua ya  kuipa Bajeti yote ofisi ya CAG kama walivyoomba kwani itaongeza ufanisi kwa ngazi ya Taifa na hata kwa Wilaya kwani wakaguzI wa ndani watakuwa na wigo mpana wa kukagua matumizi ya fedha pamoja na majengo ya serikali.

“Naishukuru na nimefurahishwa na serikali yetu kwa kuipa Bajeti yote kama ilivyoombwa na ofisi ya CAG kwani itasaidia kuongeza ufanisi wa kazi zao na pia ukaguzi utafanyika  kote kwa matumizi ya fedha na pia kukagua muonekano na ubora wa majengo ya serikali na itasaidia kupunguza hoja zisizo za lazima”.Amesema Mhe.Zainabu.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mhe. Hassan Mwinyikondo amemuahidi Mkuu wa Mkoa wa Pwani kuwa wako tayari kuungana nae ili kupata elimu na semiana mbalimbali zinazohusu masuala ya uchumi.

“ Naungana na wewe Mhe.Mkuu wa Mkoa na tupo tayari kupata elimu na semina za uchumi hata ikiwa kwa kuchangia ili waletwe wataalamu wazuri kutufundisha uchumi ili vikao vyetu vya madiwani viwe vya kiuchumi Zaidi kuliko kuangalia mapato na matumizi pekee”. Amesema Mhe

Aidha Mhe. Mwinyikondo amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zainabu Abdallah kwa kusimamia mapato kwa kuunda vikosi kazi vitatu ili kuweza na kudhibiti upotevu wa mapato.

Lengo la Baraza maalum hilo lilikuwa ni kujadili hoja mbalimbali kutoka katika Ofisi ya Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali pamoja na kufanyia kazi mapendekezo yaliopendekezwa na ofisi ya CAG.


Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.