• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Halmashauri ya Chalinze yaadhimisha Siku ya Mtoto wa Afrika kwa kushirikiana na shirika la PASADA.

Imewekwa: June 17th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii imeadhimisha siku ya Mtoto wa Afrika  katika shule ya msingi Chalinze ikiwa na kauli mbiu isemayo “Tuimarishe ulinzi wa mtoto,tokomeza ukatili dhidi yake: jiandae kuhesabiwa” ambapo kauli mbiu hiyo inaikumbusha jamii juu ya kulinda haki za watoto ilikupata jamii bora inayojali usawa na pia kusisitiza watu wote kuhesabiwa katika zoezi la sensa ya watu na makazi itakayofanyika tarehe 23 Agosti,2022 siku ya jumanne.

Katika hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Ndg.Ramadhan Possi ambaye ndiye mgeni rasmi amekabidhi vifaa nbalimbali kwa watoto wenye mahitaji maalum katika shule mbili za Msingi ambazo ni shule ya msingi Chalinze pamoja na shule ya msingi Msoga ikiwa ni ishara ya kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya jamii  katika sera yake ya kutambua umuhimu wa mtoto nchini.

Aidha Ndugu Mgeni rasmi ametoa hotuba fupi ikiwa ni mara baada ya kusomwa kwa risala kutoka kwa wananfunzi wa Shule ya msingi Chalinze ambapo amesema serikali imeendelea kuhakikisha mtoto anapata haki yake ya Msingi  ya kuishi na imechukua hatua kadhaa dhidi ya kuwakinga watoto ikiwa ni pamoja na kampeni za chanjo.

“Katika kuhakikisha kwamba mtoto anapata haki yake ya msingi ya kuishi, Serikali imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha usalama wa mama na mtoto kabla ya kujjifungua na hivyo huduma za mamam wajawazito na watoto walio chini ya miaka mitano hutolewa bure katika zahanati na vituo vya Afya. Na vilevile  Serikali  imechukua hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kampeni za chanjo ya kuzuia ulemavu utotoni kama vile polio, kutunga sharia zinazolinda maslahi na kuboresha maisha ya watoto”. Amesema Ndg. Ramadhani Possi.

Aidha Ndg.Ramadhani Possi amesema kuwa ili kuendana na kauli mbiu ya siku ya mtoto wa Afrika kwa mwaka huu 2022 Serikali na jamii haina budi kufanya mambo mbalimbali ikiwemo kuhamasisha na kuelimisha jamii juu ya haki za watoto ili kuondoa dhana potofu,kuhamasisha jami kuhusuwatoto kupata chanjo,kamati za shule ziwemstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa ujenzi wamajengo ya shule unazingatia hali za walemavu na pia kutambua matatizo,kupanga,kutekeleza,kusimamia na kutathimini miradi mbalimbali itayosaidia watoto walemavu na watoto wengine.

Nae Mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii Bi Nyamayao Said amelishukuru Shirika la PASADA kwa kushirikiana na Halmashauri ya Chalinze kwa  kuwathamini watoto katika maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambapo vifaa mbalimbali vimegawiwa kwa wanafunzi wenye uhitaji amabvyo vimegharimu jumla ya Tsh1,608,00/=.

“Niwashukuru Shirika la PASADA kwa ,kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kwa kuweza kuwafikia watoto hawa katika siku hii muhimu ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambapo  Halmashauri ya Chalinze imekabidhi vifaa kama vile sabuni,mafuta ya kupaka ,miswaki,sukari,pampasi na viburudisho vyenye thamani ya Tsh.1,208,000/= na Tsh 400,000/= kutoka Shirika la PASADA kwa jumla ya watoto 40 wenye mahitaji na changamoto ambapo watoto 20 wametoka katika shule ya Msingi Chalinze na watoto 20 kutoka shule ya msingi Msoga”. Amesema Bi.Nyamayao.

Kwa upande wa Diwani wa kata ya Pera Mhe. Jackson Mkango ameipongeza Serikali na Halmashauri ya Chalinze kwa ujumla kwa kuhakikisha inaweka mazingira mazuri ya haki na ustawi wa watoto.

Kwaniaba ya Wananchi wa Pera tumefurahi kwa maadhimisho haya kufanyika hapa na tunaishukuru Serikali na Halmashauri yetu ya Chalinze kwa kuhakikisha inaweka mazingira mazuri ya usalama, haki na ustawi kwa mtoto na kuthibitisha hilo tutamalizia ujenzi wa bweni la watoto wenye mahitaji maalumu kuanzia wiki ijayo2”.Amesema Mhe. Mkango.

Aidha Mhe. Mkango amewaomba wadau mbalimbali kushirikiana na Halmashauri ya Chalinze kuendelea kujitoa na kuunga mkono jitihada za Serikali katika kujenga na kuimarisha haki na ustawi wa watoto wetu.

Ikumbukwe kuwa Kila ifikapo Tarehe 16,juni kila Mwaka huwa ni siku ya Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambapo maadhimisho haya yalianza kuadhimishwa mnamo mwaka 1991 ikiwa ni maadhimio ya kukumbuka uasi dhidi ya wanafunzi uliotokea mnamo tarehe 16,juni,1976 huko Soweto,Afrika Kusini ikiwa na lengo la kuwakumbusha watoto hatua ya kijasiri waliyoichukua wenzao huko Afrika Kusini katika kulinda utu,heshima na haki zao za msingi.

 

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.