• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mbunge Ridhiwani: Shida ya Maji kuwa Historia Kibindu

Imewekwa: December 3rd, 2020



Shida ya Maji kwenye Vijiji na Vitongoji vya Kata ya Kibindu, Jimbo la Chalinze inatarajiwa kuwa historia kutokana na utekelezaji wa miradi ya Maji ya yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 1.6.


Awali Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akiongea mbele ya Wananchi wa Kijiji cha Kwamduma, amewahakikishia Wananchi wa Kata ya Kibindu kuwa, shida ya maji inaenda kuwa historia kwani tayari shughuli za utendaji zinaendelea.


Mbunge alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Serikali ya Awamu ya Tano kwa hatua zinazochukuliwa kupata ufumbuzi wa shida ya Maji katika kata hiyo na Jimbo zima la Chalinze.


"Serikali imejidhatiti kuhakikisha maji yanawafikia wananchi wa Kibindu. Niwahakikishie kuwa miradi hii itakamilika kwa wakati na mapema ili wananchi wapate maji safi na salama" alisema Ridhiwani Kikwete.


Pia alieza kuwa, akiwa kama Mbunge amefanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuchimbwa kwa visima zaidi ya vinne katika vijiji mbalimbali vya kata hiyo ikiwemo Kwamduma visima viwili, kibindi viwili, na Kwamsanja kimoja ambavyo vimesaidia kidogo japo shida bado haijaisha.


,"...Uchimbaji wa mabwawa haya makubwa na usambazaji kwenda kwa wananchi unakuja wakati muafaka, hivyo matarajio ni kwenda kutatua shida ya Maji kwa ukubwa huo uliokusudiwa.


Kwa hakika tuna kiongozi ambaye sio anasema mdomoni kuwajali wananchi wanyonge isipokuwa anatenda kwa vitendo pia Rais wetu Dkt. Magufuli."


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Bi. Zainab Kawawa akizungumza mbele ya wananchi wa kijiji cha Kwamduma alieleza kuwa, Serikali imejidhatiti kuhakikisha maji yanawafikia wananchi wa Kibindu hivyo alimuhakikishia Mbunge na wananchi kuwa mradi utakamilika mapema ili wananchi wapate maji safi na salama.


Akieleza juu ya Utekelezwaji wa Miradi huo, alisema Serikali imetoa Bilioni 1.6 kwa ajili ya Miradi yote ikiwemo Milioni 700 kwa ajili ya Kwamsanja na Milioni 900 kwa ajili ya Mjembe.


Ambapo miradi hiyo inatarajiwa kwa pamoja kutoa lita zisizo pungua Milioni Tatu na Nusu wingi ambao unakwenda kutatua kero ya Maji katika kata ya Kibindu.


Miradi hiyo itakapokamilika inataraji kuhudumia watu wanaoishi katika eneo la Kibindu na vitongoji vya Kata hii na za jirani.




Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.