• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mwenyekiti wa Halmashauri awapongeza walimu Chalinze

Imewekwa: May 24th, 2024

MWENYEKITI WA HALMASHAURI  AWAPONGEZA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI CHALINZE 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze,Mheshimiwa Hassani Mwinyikondo amewapongeza walimu wa Shule za Msingi katika Halmashauri ya Chalinze kwa kazi nzuri wanazozifanya za utoaji taaluma ndani ya Halmashauri ya Chalinze.


Pongezi hizo zimetolewa leo hii katika kikao kazi cha walimu wa Shule za Msingi kilichofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete. Mheshimiwa Mwinyikondo ametoa pongezi na kutoa zawadi kwa Shule zilizofanya vizuri katika katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka 2023,Shule zilizozawadiwa ni zile zilizopata wastani mzuri wa ufaulu kwa maana ya Shule tatu za Serikali na tatu za binafsi zenye ufaulu mzuri katika Halmashauri ya Chalinze,Pamoja na Maafisa Elimu kata watatu waliofanya vizuri kiwilaya.


Shule zilizopatiwa zawadi kwa upande shule za Msingi za serikali ni Mpaji ,Kibiki na Bwilingu “B”. Kwa upande wa shule za binafsi zilizopata zawadi ni Sirajul Munir Islamic,Bwani Universal Pre and Primary School na St.Alphonsa Pre &Primary School. Viwango vya zawadi kwa Shule za Serikali mshindi wa kwanza alipatiwa shilingi laki 5,mshindi wa pili laki 4 na mshindi wa tatu laki 3. Kwa Shule za binafsi mshindi wa kwanza alipata laki 3,wa pili laki 2 na mshindi wa tatu laki 1.


Mwenyekiti wa Halmashauri katika hotuba yake aliyoitoa katika kikao kazi hicho alitoa pongezi kwa shule zilizofanya vema na kuitaka Idara ya Elimu Msingi kufanya msawazo wa walimu ndani ya Halmashauri kwa kuweka usawa wa walimu walio maeneo ya mjini na vijijini ili ufaulu ukaongezeke katika maeneo yote. Hali kadhalika Mwenyekiti amezitaka shule kuweka utaratibu wa namna ya upatikanaji wa Chakula mashuleni ili kuinua kiwango cha ufaulu kwani endapo wanafunzi watapata chakula cha mchana kutatoa motisha kwa watoto kuhudhuria kikamilifu shuleni na kiongeza ufaulu.


Katika kuongeza ufaulu Mheshimiwa Mwinyikondo amewataka walimu kama walezi kuwalinda wanafunzi wao kwa kushirikiana na wazazi katika kupambana na watu wenye nia mbaya juu ya watoto wa kike ili wasipate mimba wangali bado wanasoma.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.