• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

Imewekwa: May 7th, 2025

Na John Mlyambate 


Mamlaka ya Ununuzi wa Umma Tanzania (PPRA) kwa kushirikiana na Kitengo cha Manunuzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze imetoa mafunzo ya namna ya kufuata taratibu za ununuzi wa umma kwa watumishi wa sekta ya afya ngazi ya chini. Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo watumishi hao katika kusimamia manunuzi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zinazotawala ununuzi wa umma nchini.


Mafunzo haya yamewaleta pamoja watumishi wa sekta ya afya kutoka vituo mbalimbali vya huduma ya afya ndani ya halmashauri hiyo, ambapo wamepatiwa elimu kuhusu majukumu yao katika mchakato wa ununuzi na namna bora ya kushirikiana na afisa manunuzi katika taasisi zao. Washiriki walifahamishwa pia juu ya nafasi ya PPRA kama msimamizi wa shughuli za ununuzi nchini.


Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Bi. Veronica Fute, alieleza kwa kina wajibu wa mtunza stoo katika taasisi, ikiwemo kutunza kumbukumbu sahihi za vifaa, kufanya uhakiki wa vifaa vilivyopo, na kuhakikisha vifaa vinavyohitajika vinaagizwa kwa wakati ili kuimarisha utoaji wa huduma. Alisisitiza umuhimu wa kuweka mipango mizuri ya manunuzi kulingana na mahitaji halisi ya huduma.


Bi. Fute pia alizungumzia majukumu ya idara tumizi katika mchakato wa ununuzi wa umma, akibainisha kuwa idara hizo ndizo zinazotambua mahitaji halisi ya vifaa na huduma. Hivyo, ni muhimu kwa idara hizo kushirikiana kwa karibu na maafisa manunuzi ili kuhakikisha vifaa vinavyoagizwa vinakidhi malengo ya taasisi.


Katika mafunzo hayo, washiriki walihimizwa kuzingatia maadili ya kazi kwa kuwa waaminifu, waadilifu na kuepuka mianya ya rushwa katika mchakato wa ununuzi wa umma. Bi. Fute alisisitiza kuwa ufanisi wa manunuzi unategemea kwa kiasi kikubwa uzingatiaji wa sheria na taratibu zilizowekwa na mamlaka husika.


Kwa ujumla, mafunzo haya yamelenga kuimarisha utendaji kazi wa watumishi wa afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze kwa kuhakikisha kuwa shughuli za ununuzi zinafanyika kwa uwazi, ufanisi na kwa kuzingatia matumizi bora ya fedha za umma.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.