• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Rais Samia aridhia kuanzishwa kwa mtaala wa masomo ya utalii

Imewekwa: February 10th, 2024



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kuanzishwa kwa masomo ya Utalii kwa kidato cha tano na sita nchini lengo ikiwa ni kuendelea kuikuza Sekta ya Utalii.


Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika kikao kati yake na Wabunge wa Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga kilichofanyika ukumbi wa Utawala Bungeni jijini Dodoma leo.


“Tunashukuru Mheshimiwa Rais aliona umuhimu wa kuanzishwa kwa mchepuo wa masomo ya utalii na hakuchukua muda mrefu kulikubali suala hilo” Mhe. Kairuki amesisitiza.


Amesema lengo la kuanzishwa kwa mchepuo wa masomo ya utalii ni kuendelea kuiboresha sekta hiyo akitolea mfano kutoa mafunzo ya utoaji wa huduma kwa wateja, lugha na kadhalika.


Amesema ameshawasilisha toolkit ya mchepuo huo  ambayo inaendana na matakwa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Utalii Duniani ( World Tourism Organization-UNWTO)pamoja na Wizara ya Elimu na kwamba kilichobaki ni maandalizi ya awali kwa ajili ya utekelezaji.


Aidha, katika kuboresha utoaji wa huduma kwa watalii, amesema Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kimeanza kutoa mafunzo kwa watendaji wa sekta mbalimbali wanaohusika na utoaji huduma ikiwa ni pamoja na Uhamiaji, Askari Polisi na watumishi wa sekta ya utalii.


Pia, amesema amefanya maongezi na taasisi ya  Mastercard Foundation kwa ajili ya kutoa mafunzo ya utoaji huduma na lugha ili wawe na ujuzi wa jumla na kuweza kuyazungumzia ipasavyo maeneo yao.


Kuhusu utangazaji utalii Waziri Kairuki amesema kuwa mazungumzo na taasisi mbalimbali yameshafanyika ili kushirikiana katika kutangaza utalii akitolea mfano mashirika ya ndege ya Saudia Airline,Turkish Airline, Air Tanzania Company Limited na Shirika la Kiserikali la CTG la China ambapo limeonesha nia ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania.


Katika hatua nyingine, Waziri Kairuki ameahidi kufanyia kazi mapendekezo yote katika Sekta ya Utalii ya kutangaza zaidi vivutio vya utalii, kuboresha miundombinu ya maeneo ya hifadhi, kushughulikia changamoto za wanyamapori wakali na waharibifu pamoja na masuala ya kifuta jasho /machozi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.