• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Zingatieni Sheria na Maadili ya Kazi kwa Utumishi Uliotukuka-RC Pwani

Imewekwa: May 2nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo awataka waajiri na wafanyakazi kuheshimu sheria za utumishi wa umma kwa kila mmoja kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria za nchi,ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyoadhimishwa kimkoa katika halmashauri ya Mji wa Kibaha Jana katika viwanja vya shirika la elimu Kibaha na kukemea tabia za baadhi ya waajiri wasiotaka kufuata sheria za utumishi kwa kunyanyasa wafanyakazi hatakuwa tayari kufanya kazi na watu wa aina hiyo katika mkoa wa Pwani.

Akisoma Risala ya shirikisho la wafanyakazi(TUCTA )Mkoani Pwani Bwana Ramadhani Kinyagoli aliishukuru serikali kwa jitihada zake katika shughuli za maendeleo zinazotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa maslahi ya watanzania wakiwemo na wafanyakazi,hata hivyo hakusita kuwasilisha madai na changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyakazi wa mkoa wa Pwani ikiwa ni pamoja na wafanyakazi kutopandishwa vyeo kwa wakati,kodi kubwa ya mshahara,wastaafu kutolipwa mafao yao kwa wakati,waajiri kutoheshimu sheria za utumishi kwa kutowatendea haki watumishi kwa kuwapa maslahi yao kwa mujibu wa sheria,sekta binafsi kuwazuia watumishi kujiunga na vyama vya wafanyakazi na baadhi ya halmashauri kutoitisha vikao vya mabaraza ya wafanyakazi.

Kinyangoli aliendelea kufafanua kero zinazowasibu wafanyakazi katika mkoa wa Pwani kwa kutoa shutuma kwa baadhi ya waajiri kutotimiza ahadi zao kwa wafanyakazi hodari wa mwaka jana kwa kutowapa zawadi zao hadi sasa na kuomba Uongozi wa mkoa ulifanyie kazi kwa waajiri hao kwani ahadi zisizotekelezeka kwa wakati huvunja moyo wa utendaji kazi kwa wafanyakazi wa sekta binafsi na serikali.

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo,katika hotuba yake baada ya risala ya wafanyakazi wa mkoa wa Pwani aliwapongeza wafanyakazi hodari kwa mwaka 2018 kwa utendaji mzuri hata wakaweza kuteuliwa kuwa watumishi hodari kutoka katika taasisi zao.Aliendelea kulipongeza shirikisho la wafanyakazi mkoa wa Pwani kwa risala nzuri iliyosheheni mambo mazuri na yenye tija kwa mstakabari wa utumishi nchini na kusema hakika risala hii imejaa “Nondo za kutosha”Ndikilo alisema.

Mheshimiwa Ndikilo katika hotuba yake aliahidi kuzifanyia kazi changamoto zinazo wakabili wafanyakazi ambazo ziko ndani ya uwezo wake na kwa zile zilizo nje ya uwezo wake aliahidi kuziwasilisha kunakohusika kwa hatua zaidi. Aliwataka watumishi wa serikali na sekta binafsi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni katika utumishi sanjari na maadili ya kazi kwa mujibu wa taaluma walizonazo.Aliwataka wafanyakazi kujiepusha na matendo ya utovu wa nidhamu katika kazi.”Lazima tuwe na nidhamu ya kazi uvivu kazini ni sumu katika ajira”Ndikilo alisema.

Aidha Ndikilo alisikitishwa na kitendo cha waajiri wanaotoa ahadi hewa kwa watumishi hodari na kutowatunuku zawadi zao kwa wakati hili halikubaliki hata kidogo na kutoa onyo kwa waajiri wanaobagua wananchi katika ajira hususan watu wenye ulemavu na wanawake na alisisitiza sitakuwa tayari kufanya kazi na wawekezaji wa aina hii kwani wanafanya vitu vilivyo kinyume na katiba na sheria za nchi pia.

Mwisho Mkuu wa mkoa aliwataka waajiri kuacha tabia ya kuzuia watumishi kuhama kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine ni haki ya mtumishi hivyo kukubali au kukataa uhamisho ni jukumu la wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa si suala la mwajiri.”Kama mwajiri toa maoni yako katika barua ya mtumishi na siyo kumzuia au kukataa kumpitishia barua yake ni kosa mruhusu na TAMISEMI wataamua”.Ndikilo alisema.



Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango chafanya kikao kujadili mapato na matumizi kwa mwezi Aprili 2025.

    May 31, 2025
  • Maafisa Habari watakiwa kuitangaza miradi ya serikali

    May 30, 2025
  • Halmashauri ya Chalinze yatembelewa na wawekezaji wa nyumba

    May 29, 2025
  • Kampeni ya "Ni rahisi sana"yatoa Elimu kuhushu usalama Mtandaoni Chalinze

    May 28, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.