• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mafunzo ya Teknolojia ya Vitalu Nyumba yatolewa kwa Vijana 100 Chali

Imewekwa: March 31st, 2022

Ofisi ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,imetoa mafunzo ya kilimo kwa Vijana kwa kutumia Teknolojia ya Kitalu Nyumba(Green House) kwa vijana wapatao 100 katika Halmashauri ya  Chalinze hivi karibuni.


Mafunzo hayo yametolewa katika Kijiji cha Lugoba kwa kujumuisha vijana wa kata za Bwilingu,Pera,Msoga,Lugoba,Kiwangwa,Msata na Mandela. Mafunzo haya yametolewa ili kuwajengea uwezo vijana ili kuwavutia kutafuta maarifa na kujianiri katika sekta ya kilimo na Kilimo biashara. Matumizi ya Teknolojia mbalimbali katika kilimo duniani kote yameonyesha kuwavutia vijana katika kilimo na kuwapa tija na ufanisi kibiashara.


Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze,Hassan Mwinyikondo akifunga Mafunzo hayo aliishukuru serikali ya awamu ya sita kwa jitihada zake za kuwakwamua vijana  kiuchumi kwa kuwapa maarifa wezeshi yanayowawezesha kupambana na umaskini kipitia kilimo cha kutumia Vitalu Nyumba kwa kilimo chenye tija.


Mwinyikondo aliwataka Vijana kuyatumia maarifa waliyoyapata kwa weledi na kwa faida yao na jamii kwa ujumla ili kujikwamua kiuchumi ili kufikia azima ya serikali na ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa Ujumla.


Katika hotuba yake ya kuhitimisha mafunzo Mwenyekiti aliwataka vijana wahitimu kujiunga katika vikundi ili halmashauri iweze kuwapatia mikopo ya kujenga vitalu nyumba kutokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

“Mafunzo haya yakawe chachu ya mafanikio na maarifa mliyoyapata mkayatumie kwa vitendo na kuwawezesha pia vijana wenzenu ambao hawajayapata mafunzo haya na hatimaye mkapate mikopo ambayo itatumika katika kilimo cha vitalu nyumba.”Mwinyikondo alisema.


Naye Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika,Bwana Jovin Bararata aliishukuru Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kutoa mafunzo kwa vijana kuhusu Kilimo cha Kisasa na utumizi wa Vitalu nyumba kwa kilimo chenye tija ,hali ambayo itawafanya vijana kukipenda kilimo kinachotumia teknolojia ya kitalu nyumba kwa uzalishaji wenye tija.


Aidha Bararata aliahidi kuwa mafunzo haya yatakuwa endelevu kwa vijana ili waweze kupambana na umasikini kupitia teknolojia ya kilimo inayotumia vitalu nyumba.

“ Idara ya kilimo tunaahidi kuendelea kuwajengea uwezo vijana juu ya utumizi wa vitalu nyumba katika Halmashauri ya Chalinze kwa kuhakikisha kila kata Teknolojia hii inatumika kwa ufasaha ili kuwavutia vijana kukipenda kilimo kama mkombozi katika jamii.” Bararata alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze akifunga Mafunzo kwa Vijana 

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.