• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Chalinze DC yafanya Kikao cha Baraza Maalum la Bajeti 2022/2023.

Imewekwa: January 24th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze imefanya kikao chake cha baraza maalum la  bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo Baraza lapitisha Bilioni 48.09 kwa mwak wa fedha unaoanza  na kuweka kipaumbele katika sekta ya afya ,elimu na Miundombinu.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mhe. Hassan Rajabu Mwiinyikondo ameeleza ni ni kwa namna gani bajeti hiyo ya Shilingi Bilioni 48.09 imegusa sekta muhimu na zenye kipaumbele kwa jamii na kuamini zitatatua kero za wananchi wa Halmashauri ya Chalinze ambapo alisema,

“Katika bajeti hii vipaumbele tulivyoviweka vimegusa mpango mkakaki wa Serikali  kwasababu mpango mkakati wa Serikali ni kuiwezesha sekta za afya,elimu na miundombinu hivyo basi katika Bajeti hii ya 2022/2023 naamini inakwenda kutatua changamoto zote za  wananchi wetu” Alisema Mhe. Mwiyikondo.

Hata hivyo Mhe. Mwinyikondo amelipongeza baraza la Madiwani kwa kupitisha Bajeti hiyo kwa mwaka wa fedha ujao kwani ni bajeti inayobeba vipaumbele muhimu kwa jamii naTaifa ili kuondoa kero za wananachi na kuwaahidi kufanya kazi kwa ushirikiano baina ya watendaji na madiwani wa Halmashauri ya Chalinze.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Ndg. Ramadhan Possi ametoa shukrani kwa Waheshimiwa Madiwani kwa kupitisha bajeti hii ya Bil. 48.09 kwa mwaka wa fedha ujao na kubainisha miradi ya kimaendeleo itakayoanzishwa katika Halmashauri ya Chalinze.

“ Niwashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa kupitisha bajeti yetu kwa mwaka unaokuja na katika bajeti hii tumeweka vipaumbele katika Miradi ya maendeleo kwa sekta ya elimu tumetenga bajeti ya Shiling Mil.300 na sekta ya  Afya tumetenga fedha Shilingi Milioni 400 kwaajili ya Hospitali ya Wilaya iliyopo. Alisema Ndg. Possi.

Vilevile MkurugenziMtendaji aliongeza kwa kusema kuwa Halmashauri imetenga fedha kwaajili ya miradi ya Kimkakati ikiwa ni pamoja na maegesho ya magari makubwa,ujenzi wa masoko maeneo mbalimbali na kituo cha Mabasi (Chalinze Bus Stand).

 “Kama Halmashauri pia tumeweza kutenga bajeti kwa miradi ya kimkakati ikiwa kwanza Chalinze tuna ukosefu wa maegesho ya magari makubwa mpaka kusababisha magari kuzagaa hovyo hivyo basi tumetenga fedha kwaajili ya  ujenzi wa maegesho ya magari makubwa lakini pia Halmashauri tumeanzisha soko katika kata ya Bwilingu ambapo tumeanza kwa hatua ya kwanza na kwa bajeti ya mwaka ujao tumelitengea fedha kwa ujenzi wa awamu ya pili na kwa upande wa kata za Lugoba na Msata tumetenga kiasi cha Shilingi Milioni 200 kwa mgawanyo wa Milioni 100 kwa kila Kata na Kubwa zaidi ni Ujenzi wa kituo cha Mabasi (Chalinze Bus Stand) kwawa awamu ya kwanza na kituo hicho  kimeanza kufanya kazi na kwa awamu ya pili tunatenga pesa kwaajili ya kuwezesha kituo cha mabasi kiweze kukamilika ipasavyo”. Alisema Ndg. Possi.

Ikumbukwe kuwa Miradi ya kimkakati yote iliyoanza kufanywa na ambayo imepangwa kufanywa inatumia pesa za mapato ya ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.