• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Chanjo ya kuzuia Saratani ya Mlango wa Kizazi yazinduliwa rasmi Chalinze

Imewekwa: May 1st, 2018

Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo,Alhaj Majid Mwanga amezindua rasmi kampeni ya chanjo ya kuzuia Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa watoto wa kike waliofikia umri wa miaka 14,uzinduzi huo umefanyika jana katika kijiji cha Kikaro kata ya Miono katika halmashauri ya wilaya ya Chalinze.Kampeni hizi ni mkakati wa serikali ya awamu ya tano katika kupambana na ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi ambao umekuwa tishio kwa afya za wanawake hapa nchini na ulimwenguni kote kwa ujumla.

Kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo kulitolewa mafunzo kwa wadau na wahamasishaji wa masuala ya afya ya msingi katika jamii kwa maana ya wahudumu wa afya,maafisa watendaji wa vijiji na kata,maafisa tarafa,maafisa maendeleo ya jamii,viongozi mbalimbali wa dini na walimu wa shule za msingi na sekondari ili wapate ufahamu kuhusu saratani ya mlango wa uzazi,dalili za maabukizi ya virusi vya “Human Pappiloma Virus”(HPV),dalili za saratani ya mlango wa kizazi,chanjo ya kukinga Saratani ya mlango wa kizazi,namna inavyotolewa chanjo na maudhi madogo madogo yanayoweza kutokea baada ya chanjo kwa watoto.

Katika mafunzo hayo Mganga Mkuu wa halmashauri ya wilaya Dkt.Rahim Hangai aliwataka washiriki kuwa mabalozi katika kufanikisha zoezi hili muhimu la kitaifa ili kuwanusuru watoto wa kike wasipatwe na virusi vya HPV na kupelekea kupatwa na saratani ya mlango wa kizazi ugonjwa ambao ni hatari na unaua wanawake wengi katika nchi zinazoendelea.

Naye Mratibu wa chanjo wa wilaya Ally Msopa,akitoa mada kwa washiriki aliwaeleza umuhimu wa chanjo ya HPV kuwa inakinga maambukizi ya virusi vya HPV vinavyosababisha saratani ya mlango wa kizazi na inatolewa mara mbili ili kupata kinga kamili,chanjo hii inaweza kupunguza matukio ya saratani ya mlango wa kizazi kwa kiwango kikubwa.Chanjo hii ni salama,imethibitishwa na Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Wazee na Watoto na Shirika la afya Duniani.

Aidha Msopa alifafanua baadhi ya dalili za awali  za maabukizi ya virusi vya HPV kuwa ni vivimbe sehemu za uke au uume vijulianavyo kama viotea,dalili za baadaye ni mabadiliko katika seli za mlango wa kizazi na mabadiliko haya yasipodhibitiwa mapema hugeuka kuwa saratani ya mlango wa kizazi au viungo vingine.

Kwa upande wake kiongozi wa dini ya kiislamu Sheikh Hamis Nassor kwa niaba ya viongozi wa dini alisema tumepokea mkakati huu wa serikali kwa mikono miwili tutahamasisha jamii kwa nguvu zote ili kuwanusuru mabinti zetu na janga la saratani ya mlango wa kizazi, na kila changamoto itakayojitokeza tutakabiliana nayo.”Naomba Mungu awajalie viongozi wetu afya njema umri wenye tija katika kulitumikia taifa”.Sheikh Nassor alisema.

Mkuu wa wilaya katika hotuba yake ya uzinduzi wa kamapeni ya chanjo ya kuzuia Saratani ya Mlango wa Kizazi aliwataka watumishi wa idara ya afya kuwa na moyo wa uzalendo na wa kujitolea ili zoezi hili liweze kufanikiwa kwani kuna zahanati ambazo hazina watumishi wa afya na vijiji vingine havina kabisa zahanati, hivyo alimtaka Mganga wa Halmashauri kuendesha zoezi hili kwa njia ya huduma ya Vikoba (Out Reach Services)kwa kupanga ratiba za kuwafikia wananchi katika maeneo yao kwa muda mahsusi ili tuweze kukamilisha zoezi hili kwa asilimia 100.Baada ya nasaha zake alizindua rasmi kampeni ya chanjo kwa watoto wa kike wote waliofikia umri wa miaka 14.




Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • TANGAZO LA KAZI June 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Waziri Kikwete Apokea Hundi ya Tsh Milioni 52 kutoka kiwanda cha Keda

    June 21, 2025
  • Chalinze yapongezwa kwa Hati Safi Mfululizo miaka mitano

    June 18, 2025
  • Mwenyekiti wa UWT akagua miradi ya maendeleo Chalinze

    June 13, 2025
  • Madiwani wa Pangani waipongeza Chalinze kwa Miradi ya mapato ya ndani

    June 11, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.