• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mh Ridhiwani Kikwete (Mbunge) akabidhi Pikipiki, Bajaji na TOYO kwa kikundi cha Wazalendo

Imewekwa: June 11th, 2021

Hayo yamejili leo katika viwanja vya Halmashauri  kwenye hafla fupi ya Makabidhiano ya vifaahivyo vya usafirishaji kati ya Uongozi wa Halmashauri na Kikundi cha Wazalendo kutoka kata ya Msata, Mbunge huyo alikabidhi Pikipiki, Bajaji na TOYO ya kubebea mizigo zenye  dhamani ya Tsh 48,384,500/= ikiwa ni sehemu ya marejesho ya asilimia kumi(10%) kwa makundi ya vijana, kinamama na walemavu kutoka katika makusanyo ya mapato ya ndani.

Akito neno la utangulizi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze Ndugu Ramadhani Possi alisema, Kwa sasa Halmashauri imeamua kujikita katika kusaidia Makundi haya maalumu ili kuyainua Zaidi kiuchumi,

Tumeona tujikite Zaidi katika uwezeshaji wa Vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kupitia uanzishaji wa Miradi Mkakati, Kwa Mwaka huu tumefanikiwa kuviwezesha vikundi vinavyojihusisha na Usindikaji wa Matunda, Utengenezaji wa Samani za Mbao, ufugaji wa kuku wa kisasa na Usafirishaji kutoka kata ya Miono, Msata, Kiwangwa, Bwilingu na Pera. Alisema Ndugu Ramadhani Possi 

Hatujafanikiwa sana kwa kundi la watu wenye ulemavu kutokana na sharia iliokuwepo ilitaka wajikusanye kundi la watu wasiopungua watano ndio wapewe mkopo ila tunaamini kwa mwaka ujao wa fedha tutafanya vizuri kwani sharia hiyo imerekebishwa na inamruhusu hata Mtu mmoja kukopa katika kundi hili la watu wenye ulemavu. Aliongeza Ndugu Ramadhani Possi

Nae Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete alimshukuru Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Ismail Msumi na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kwa ajili ya kufanikisha swala la urejeshaji wa 10% kwa makundi hayo muhimu nakuwataka waendelee na utendaji huo.

Aidha Mh Mbunge aliongeza kwa kuwapongeza wanakikundi cha WAZALENDO kwa niaba ya vikundi vyote vilivyopokea mkopo na kuwataka kuhakikisha wanasimamia biashara zao vizuri na kurejesha fedha hizo kwa wakati ili na vikundi vingine vinufaike kama wao walivyopata fedha hizo.

 

Serikali kupitia uongozi wa awamu ya sita chini ya Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan inawapenda vijana na diomaana inaweka mkazo kwenye mikopo hiyo, hivyo kwa kutumia kipato watakachopata waimarisha Maisha yao kiuchumi, kwani hata katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha vitu vingi vimeshuka kwa lengo la kumuinua mwananchi maskini aweze kuimarika kimaisha na kiuchumi.

Mbunge wa jimbo la Chalinze alihitimisha kwa kumuagiza Mkurugenzi Mtendaji Ndugu: Ramadhani Possi kuona namna ya kuwaongezea muda wa marejesho kwa mwezi mmoja kikundi hicho cha Wazalendo kwani tangu wamesaini mkataba wa kukabidhiwa mkopo huo umepita mwezi hadi kukabidhiwa vifaa hivyo, Kama kutahijika maamuzi ya vikao basi aone namna ya kuharakisha mchakato huo ili vijana waweze kunafaika zaidi kwa kupata muda wa kutosha kuvifanyia kazi vifaa kabla ya kuanza marejesho sawasawa na miongozo inavyotaka.


PICHA ZA TUKIO LA KUKABIDHI VYOMBO VYA USAFIRI KWA KIKUNDI CHA WAZALENDO KILICHOPO KATA YA MSATA



Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete Akimvisha Kofia Ngumu

deleva wa Toyo wa kikundi cha WAZALENDO  ikiwa ni ishara ya kukabidhi rasmi

vifaa hivyo kwaajili ya kuanza Kutumika.



Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete (Aliesimama Mkono wa Kulia)

na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. Ismail Msumi wakikata utepe kwa pamoja 

katika uzinduzi wa Hafla ya makabidhiano ya Mradi wa usafirishaji kati ya Kikundi cha 

Wazalendo na Uongozi wa Halmashauri



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chalinze akitoa maelezo kuhusiana na Mradi 

mkakati ambao kupitia 10% ya mapato ya ndani Halmashauri imewawezesha vijana wa 

kikundi cha Wazalendo mbele ya Mbunge,Madiwani na Wageni waarikwa kwenye Hafla

 hiyo.




Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.