• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Divisheni ya Miundombinu,Maendeleo ya Vijijini na Mijini
      • Divisheni ya Elimu ya Awali na Msingi
      • Divisheni ya Elimu ya Sekondari
      • Divisheni ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Kitengo cha Udhibiti wa Taka ngumu
      • Kitengo cha Maliasili na Hifadhi ya Mazingira
      • Kitengo Cha Fedha na Uhasibu
      • Divisheni ya Mipango na Uratibu
      • Divisheni ya Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Divisheni ya Maendeleo ya Jamii
      • Divisheni ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
      • Divisheni ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Kitengo cha Usimamizi wa Ununuzi
      • Kitengo cha Michezo,Utamaduni na Sanaa
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Huduma za Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
    • MATANGAZO
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mhe. Mwinyikondo athibitishwa na kuapa Rasmi

Imewekwa: December 13th, 2021

Waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mkoa wa Pwani hii leo wamemthibitisha Mhe. Hassan Mwinyikondo diwani wa Kata ya Msoga kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze akichukua nafasi ya Mhe Godfrey Kamugisha.

Zoezi hilo lilifanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chalinze ambapo madiwani walipiga kura za ndio au hapana  kwa  jina moja lililopitishwa na chama ambapo Mhe. Mwinyikondo alipigiwa kura zote za madiwani waliokuwepo na kuapishwa mbele ya  Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Mhe.Hashim na baadae kamati ya Uchumi na Mazingira imemchagua Mh.Malota Kwaga  Diwani wa kata ya Kiwangwa kuwa Mwenyekiti wa kamati ya Uchumi na Mazingira ili kujaza nafasi ya mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Halmashauri.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bagamoyo Mhe.Shariff Zahoro  amempongeza Mwenyekiti Mpya wa Halmashauri ya Chalinze kwa kuchaguliwa kuiongoza Halmashauri hiyo na kuwataka Waheshimiwa madiwani na Watendaji kutoa ushirikiano.

Nikupongeze kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti na niwapongeze madiwani wote waliokuchagua wewe na inaonesha mna ushirikiano mzuri kwani wamekupigia kura zote lakini pia ninaomba nikupe nasaha zangu kwako ni kusimama imara kwa kuhakikisha Halmashauri inakwenda kwa kasi kubwa sana kwani Chama ,Madiwani na Watendaji wana imani na wewe na ukafanye kazi kwa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato ili Chalinze iende mbele vilevile niwaombe Waheshimiwa Madiwani na Watendaji  mumpe ushirikiano,na ushauri mzuri Mwenyekiti wetu mpya lakini pia kuwepo na mshikamano madhubuti ili jahazi la Halmashauri ya Chalinze linafika salama”.Alisema Mhe.Shariff.

Aidha Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Zaibabu Abdallah amempogeza Mhe. Mwinyikondo kwa kupewa dhamana ya kuwa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze na kumshauri Mwenyekiti mpya wa Halmashauri mambo matatu muhimu yatakayosaidia kuiongoza vyema Halmashauri ikiwemo mapato na matumizi,kusimamia miradi na Kuwa kiunganishi.

“  Nichukue fursa hii kwaniaba ya ofisi ya Wilaya  kumpongeza Mhe. Mwinyikondo kwa kuchaguliwa na Chama kwa kura nyingi na kuthibitishwa na Madiwani kwa kishindo na hii inaonesha Waheshimiwa madiwani wana imani na wewe lakini pia binafsi nimeona kazi kubwa unayoifanya na katika ushauri wangu Mhe. Mwenyekiti ninaomba uzingatie mambo haya matatu ikiwemo usimamizi wa mapato na matumizi ikiwa huu ndio msingi mkuu wa Halmashauri na ikizingatiwa kwa mwaka huu tumepanga kukusanya Bilioni 10.7 hivyo niombe hakikisha tunakusanya mapato na tunavuka malengo, pia tunamshkuru mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea fedha za UVIKO-19 zaidi ya Bilioni moja kwaajili ya ujenzi wa madarasa hivyo basi  ukasimamie miradi hii kwa nguvu zako zote na kwakuwa umeapishwa na kuthibitishwa leo tunaomba tuungane mimi pamoja na kamati ya usalama kukagua miradi hiyo ya madarasa kuona miradi hiyo inaendelea vyema na kuona thamani ya ujenzi inakidhi ili kufikia tarehe 30/12/2021 miradi hiyo iwe imekamilika kama ilivyoelekezwa na  TAMISEMI, jambo la pili  ni kusimamia vyema miradi ya huduma za jamii ili kuona fedha inatumika kwa usahihi na pia usimamie miradi yote ikiwemo TFS,DAWASA,RUWASA na TANESCO na jambo la tatu ni kuwa kiunganishi kati ya Halamshauri na Chama Cha Chapinduzi,halmashauri na serikali kuu kwa kushirikina na kuwa kiunganishi kati yako Mwenyekiti na Halmashauri kwa maana ya madiwani wote wa Chalinze” Alisema Mhe. Zainab Abdallah.

 “Lakini pia niwashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa kupitia Mwenge wa Uhuru Wilaya yetu imepata bahati ya kuwa wa kwanza Kimkoa,watatu kikanda na wa sita Kitaifa na hiyo yote ni ushirikiano wa Madiwani mpaka kufika hapa, hivyo kwaniaba ya Serikali ninawashukuru sana kwa ushirikiano katika kuweka heshima kubwa kimkoa na nina imani kwa mwaka ujao tutajitahidi ili ikimpendeza Mungu tuwe wa Kwanza Kitaifa.” Aliongeza Mhe. Zainabu Abdallah.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze Mhe. Hassan Mwinyikondo ametoa neno la Shukrani kwa Chama Chama Cha Mapinduzi,Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya na Madiwani wote kwa dhamana aliyopewa

Kutoka ndani ya moyo wangu ninashukuru Chama Cha Mapinduzi CCM, Mkuu wa Wilaya Pamoja na Madiwani kwa dhamana kubwa sana mliyonipa ya kuisimamia Halmashauri ya Chalinze na ninawaahidi sitowaangusha na ninapenda kusema Uchaguzi umekwisha hivyo basi sisi madiwani wote tuungane na tushirikiane kuhakikisha Halmashauri inakwenda kwani tumepokea nasaha kutoka kwa viongozi mbalimbali na kwa Chama chetu cha Mapinduzi CCM na kwa Mkuu wa Wilaya na ninahakikisha nasaha hizo tunazifuata

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA February 03, 2025
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • PPRA yatoa Mafunzo ya NeST kwa Watendaji wa Kata na Wakuu wa Shule Chalinze

    May 08, 2025
  • Watendaji wa Kata na Vijiji wapewa Mafunzo ya namna ya kukusanya Kodi ya Majengo Chalinze

    May 07, 2025
  • PPRA yatoa mafunzo ya Ununuzi kwa watumishi wa Afya Chalinze

    May 07, 2025
  • Kamati ya Fedha,Uongozi na Mipango yafanya ziara kukagua miradi ya maendeleo

    May 06, 2025
  • Tazama zote

Video

Ofisi ya Utumishi yakutana na Watumishi wa ajira mpya Chalinze
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • mfumo wa taarifa wa kiutumishi (ess)
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2020/2021
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • Mamlaka ya Serikali Mtandao
  • Jinsi ya Kusajili na kupata namba ya mlipakodi (TIN NAMBA)
  • mfumo wa mrejesho serikalini
  • mfumo wa manunuzi wa umma

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    114 Morogoro Rd, 61383 Bwilingu

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.