• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
    • Maoni |
Chalinze  District Council
Chalinze  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halimashauri
    • Idara
      • Rasilimali watu na utawala
      • Elimu msingi
      • Elimu secondari
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Maji na umwagiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Mipango Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Ardhi na maliasili
      • Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Vijana
      • Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji
      • Ujenzi
    • Vitengo
      • Tehama na Uhusiano
      • Ufugaji Nyuki
      • Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
    • Utaalamu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Utawala na Mipango
      • Afya,Elimu na Maji
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Maadili
      • VVU/UKIMWI
    • Ratiba ya Vikao
    • Shughuli za Maendeleo za Madiwani
      • Kata ya Bwilingu
      • Kata ya Kibindu
      • Kata ya Kimange
      • Kata Kiwangwa
      • Kata ya Lugoba
      • Kata ya Mandera
      • Kata ya Mbwewe
      • Kata ya Mkange
      • Kata ya Msata
      • Kata Msoga
      • Kata ya Pera
      • Kata ya Tarawanda
      • Kata ya Ubenazomozi
      • Kata ya Vigwaza
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Service Client Charter
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Hatua
    • Miongozo
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video za shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Maendeleo ya Jamii jinsia na Vijana


IDARA YA  MAENDELEO YA JAMII NA USTAWI WA JAMII

Idara ya maendeleo ya jamii  na ustawi wa jamii ni moja ya kati ya idara  13 zilizo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Jukumu kubwa la Idara ni kuiwezesha Jamii kuweza kutambua mahitaji  na matatizo yake yenyewe na kuchukua hatua za kubaini  ufumbuzi wa matatizo au mahitaji  yake kwa kutumia rasilimali zilizopo ndani na nje

MUUNDO WA IDARA

Idara ya maendeleo ya jamii  na ustawi wa jamii imegawanyika katika vitengo 7 ambavyo hufanya kazi kwa ushirikiano ili kuhakikisha maendeleo ya wananchi yanapatikana, vitengo hivyo ni pamoja na:-

1.    Mipango utafiti na Takwimu

2.    Maendeleo ya wanawake na Dawati la jinsia

3.    Maendeleo ya vijana

4.    Ustawi wa jamii na watoto

5.    Ukimwi

6.    Uratibu wa Asasi zisizo za kiserikali(NGOs)

7.    Dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi

MAJUKUMU YA VITENGO NDANI YA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII

1. MIPANGO UTAFITI NA TAKWIMU

  • Kuratibu uandaaji wa mipango na bajeti ya idara
  • Kuandaa taarifa za utekelezaji wa mipango na bajeti ya idara pamoja na taarifa nyingine
  • Kuratibu taarifa za tafiti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuzitumia katika mipango ya idara na machapisho mengine
  • Kuratibu upatikanaji wa takwimu na tafsiri za takwimu katika matumizi mbalimbali ya idara na sekta nyingine.

2. MAENDELEO YA WANAWAKE  NA DAWATI LA JINSIA

  • Kuratibu usimamizi wa mfuko wa maendeleo ya wanawake
  • Kuratibu upatikanaji wa fursa mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kiutawala kwa maendeleo ya wanawake
  • Kuratibu dawati la jinsia kwa kuhakikisha mpango wa jinsia katika wilaya unazingatiwa na kutekelezwa.

3. MAENDELEO YA VIJANA

  • Kuratibu na kisimamia utekelezaji wa Sera ya Vijana
  • Kuratibu shughuli za mikopo/mifuko ya Vijana
  • Kuhamasisha vijana ili kufufua moyo wa kujitolea nchini
  • Kupanga na kuendesha mafunzo yanayohusu stadi za maisha, stadi za kazi na Afya ya Vijana
  • Kuanzisha vituo vya ushauri nasaha, Ajira kwa Vijana na Elimu ya Familia kwa kushirikiana na vyama visivyo vya kiserikali (NGO)
  • Kukusanya takwimu mbalimbali zinazohusu Vijana
  • Kuratibu shughuli mbalimbali za NGO zinazoshughulikia masuala ya Vijana
  • Kuandaa mipango ya kuboresha malezi ya Vijana
  • Kuwahamasisha Waajiri na Wafadhili mbalimbali wachangie mfuko wa mikopo nafuu kwa Vijana katika maeneo mbalimbali
  • Kukuza na kuendeleza vipaji mbalimbali walivyonavyo Vijana ili kuwawezesha kujiajiri
  • Kuandaa mipango ya kuwahamasisha Vijana ili kuanzisha miradi midogomidogo ya kujiajiri.

4.USTAWI WA JAMII NA WATOTO

  • Kuendesha usahili kwa wahudumiwa(watu wenye ulemavu,wazee,familia zenye matatizo pamoja na watoto na vijana wenye matatizo mbalimbali)
  • Kuandaa taarifa za usaili na ukaguzi wa mazingira ya wahudumiwa
  • Kufanya ukaguzi wa mazingira wanayoishi wahudumiwa ili kupata taarifa zao kamili
  • Kupokea na kukusanya taarifa za ustawi wa jamii kutoka kwa wadau na vituo mbalimbali vya ustawi wa jamii.
  • Kupokea na kukusanya takwimu zinazohusu huduma za watu wenye ulemavu, wazee malezi ya watoto na familia zenye matatizo.
  • Kupokea kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya uandikishaji wa vituo vya kulelea watoto wadogo mchana, malezi ambao (foster care) na vyuo vya malezi vya watoto wadogo mchana.
  • Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya msaada wa Rais kutoka kwa akina mama waliojifungua watoto watatu au zaidi kwa mara moja.
  • Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi ya watoto yatima au wanaohitaji misaada mbalimbali.
  • Kupokea, kuchambua na kuandaa orodha ya maombi mbalimbali kutoka kwenye familia na watu wenye dhiki.
  • Kuhoji na kuandaa taarifa za washtakiwa.

5. UKIMWI

  • Kuratibu, Kupanga  na kusimamia shughuli zote za VVU na UKIMWI ngazi ya wilaya, Mji.
  • Kushirikiana na mratibu wa UKIMWI sekta ya afyakatika utekelezaji wa afua za UKIMWI na kukusanya takwimu za UKIMWI katika halmashauri
  • Kushirikiana na wadau wa ukimwi kuandaa mipango ya utekelezaji wa afua za ukimwikupitia zana ya kuandaa mpango mkakati wa mkoa
  • Kuandaa taarifa za utekelezaji wa shughuli za ukimwi za robo, nusu na mwaka mzima na kuziwasilisha ngazi ya halmashauri, Mkoa na wadau husika
  • Kusimamia na kuratibu shughuli za waratibu wa ukimwina waelimisha rika katika idara za halmashauri
  • Kubaini mahitaji na kuandaa mpango kazi wa kujenga uwezo miongoni mwa wadau wanaojishughulisha na afua za ukimwikatika halmashauri
  • Kukusanya na kuunganisha taarifa kutoka kamati za ngazi ya kata  na mtaa/vijiji
  • Kuwezesha na kuzijengea uwezo kamati na wadau mbalimbali wa VVU na UKIMWI
  • Kufuatilia na kutathmini shughuli za VVU na UKIMWI katika halmashauri
  • Kuandaa kikao cha wadau wa afua za VVU na UKIMWI kila robo ya mwaka
  • Kufuatilia na kutathimini vichocheo vya maambukizo ya VVU yanayotokana na madawa ya kulevya.

6. URATIBU WA ASASI ZISIZO ZA KISERIKALI (NGOs)

  • Kuratibu kazi na ripoti za taasisi za kijamii zilizopo wilayanikwa kuhakikisha shughuli zote za taasisi zinafuata muongozo wa taasisi za kijamii
  • Kuwezesha usajili wa taasisi zote za kijamii zisizo za kiserikali
  • Kutoa ushauri kwa taasisi za kijamiikatika kutekeleza majukumu yake ikiwa ni pamoja na kuzingatia miongozo ya kisekta

7. DAWATI LA UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI

i.     Kusimamia na kufuatilia shughuli za uwezeshaji zinazofanywa katika kata na vijiji/mitaa katika Halmashauri

ii.    Kutafsiri na kusimamia utekelezaji wa Sera na Sheria ya Taifa ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Mkakati wa Taifa wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi katika Halmashauri

iii.    Kukusanya taarifa na tafi ti mbalimbali na kumshauri Mkurugenzi wa Halmashauri katika masuala ya uwezeshaji kiuchumi

iv.    Kuhakikisha fedha za uendeshaji zinatengwa katika bajeti kila mwaka kwa ajili ya masuala ya uwezeshaji

v.    Kuhakikisha kuwa Halmashauri inahusisha suala la hifadhi ya Mazingira na mabadiliko ya Tabia Nchi katika Mipango ya Maendeleo ya Wilaya ili kuboresha mazingira ambayo ni muhimu katika suala zima la uzalishaji mazao ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi

vi.    Kubuni na kutafuta vyanzo vya rasilimali kwa ajili ya shughuli za uwezeshaji katika Halmashauri yake

vii.    Kuratibu na kuhamasisha uanzishwaji na uendelezaji wa vikundi vya kiuchumi kama SACCOS, VICOBA na vingine vinavyosajiliwa na kutambuliwa toka ngazi ya wilaya hadi taifa

viii.    Kuwasilisha taarifa ya utekelezaji kwa Kamati ya Uwezeshaji ya Halmashauri na baada ya kuidhinishwa itumwe kwa Mratibu wa Uwezeshaji Mkoa na nakala kwa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi

ix.    Kuhamasisha vikundi vya kijamii na kiuchumi kujisajili/kujirasimisha na kufanya uzalishaji wenye viwango vya TBS, TFDA na kupata nembo ya utambuzi wa bidhaa (msimbomilia (Barcode))

x.    Kuandaa taarifa ya maendeleo ya vyama vya ushirika hasa SACCOS na vikundi vya kiuchumi kama VICOBA vilivyopo katika Halmashauri

xi.    Kubuni fursa mbalimbali za uwekezaji katika Halmashauri; xii. Kufuatilia upatikanaji wa masoko ya bidhaa za kiuchumi

xii.    Kushauri namna ya uboreshaji wa vituo vidogovidogo vya kibiashara, hususan, katika vijiji na Mamlaka za Miji Midogo.


Katika kukabiliana na changamoto za utandawazi na mabadiliko ya mila na desturi,  maisha ya mwanadamu na Jamii kwa ujumla yamekuwa yakikabiliwa na changamoto nyingi za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Hivyo njia pekee ya kukabiliana na changamoto hizi ni kuhakikisha  Jamii inashirikishwa ipasavyo katika kukabiliana na utatuzi wa changamoto zake zenyewe. Katika hili Idara ya Maendelea ya Jamii na Usatawi wa Jamii ni daraja muhimu.



Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE CSEE 2018 January 24, 2019
  • TANGAZO LA MKUTANO WA BALAZA LA MADIWANI ROBO YA NNE August 28, 2019
  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA MKOA WA PWANI December 18, 2018
  • TANGAZO LA KUSITISHWA KWA UHAMISHO August 31, 2018
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mafunzo ya Kuwajengea Uwezo Madiwani Yatolewa Chalinze

    December 21, 2020
  • Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Bagamoyo Yaridhia Chalinze kuwa Wilaya.

    December 19, 2020
  • Madiwani waridhia Kuanzishwa Wilaya Mpya ya Chalinze

    December 18, 2020
  • Baraza la Madiwani Chalinze Limezinduliwa

    December 18, 2020
  • Tazama zote

Video

Waziri OR-TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo akihimiza ukusanyaji Mapato kwenye mamlaka za serikali za Mitaa
Video nyingine

Viungio vya haraka

  • Mfumo wa Kiuhasibu wa Kuripoti fedha katika Vituo (FFARS)
  • Mfumo wa Bajeti
  • RIPOTI YA MKAGUZI MKUU WA SERIKALI 2015/2016
  • WAZO LA WAZIRI
  • Mfumo wa Vibali vya Kusafiri Nje ya Nchi
  • JINSI YA KUJISAJILI NA KUPATA NAMBA YA MLIPA KODI (TIN NAMBA)

Viungio vya tovuni mhimu

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
  • Tovuti ya Mkoa
  • Tovuti ya Serikali
  • Tovuti ya Utumishi
  • Baraza la Mitihani la taifa
  • Tovuti ya Sekretarieti ya Ajira

Wasomaji Mbalimbali Dunia

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

Visitors Counter

Ramani ya eneo

Wasiliana nasi

    Lugoba Chalinze

    Anuani ya posta: P O BOX 65 Chalinze

    Simu: +255232935403

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe : ded@chalinzedc.go.tz

Anwani Nyingine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Copyright ©2018 chalinze district council . All rights reserved.